TIMU yetu ya wanawake ya Yanga Princess leo itashuka kwenye uwanja wa Uhuru, jijini Dar Es Salaam majira ya saa 10:00 jioni kupambana na Alliance Girls.
Huu ni mchezo wa nne kwa Princess kwenye Ligi Kuu ya wanawake msimu huu, wakishika nafasi ya 5 baada ya kujikusanyia pointi 4.
Alliance Girls wako nafasi ya 4 wakiwa na pointi 7 baada ya kushinda mechi mbili na kutoka sare mchezo mmoja.
Princess wenyewe wameshinda mchezo mmoja dhidi ya Mkwawa Queens kwa bao 4-0, kisha kupata sare ya bao 1-1 kwenye Derby dhidi ya Simba Queens na wamepoteza kwa bao 1-0 mbele ya Fountain Gate.
Mchezo huu hautakuwa na Kiingilio na utaonyeshwa Mbashara kupitia YANGA APP na YANGA TV inayopatikana kwenye mtandao wa YouTube.
The Young Princess team does well, more efforts should be done to make players more talented